Zaburi - Sura 87

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150
← Iliyotangulia Inayofuata →
1 Msingi wake upo Juu ya milima mitakatifu.
2 Bwana ayapenda malango ya Sayuni Kuliko maskani zote za Yakobo.
3 Umetajwa kwa mambo matukufu, Ee Mji wa Mungu.
4 Nitataja Rahabu na Babeli Miongoni mwao wanaonijua. Tazama Filisti, na Tiro, na Kushi; Huyu alizaliwa humo.
5 Naam, mintarafu Sayuni itasemwa, Huyu na huyu alizaliwa humo. Na Yeye Aliye juu Ataufanya imara.
6 Bwana atahesabu, awaandikapo mataifa, Huyu alizaliwa humo.
7 Waimbao na wachezao na waseme, Visima vyangu vyote vimo mwako.
← Rudi kwenye faharasa