Zaburi - Sura 3

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150
← Iliyotangulia Inayofuata →
1 Bwana, watesi wangu wamezidi kuwa wengi, Ni wengi wanaonishambulia,
2 Ni wengi wanaoiambia nafsi yangu, Hana wokovu huyu kwa Mungu.
3 Na Wewe, Bwana, U ngao yangu pande zote, Utukufu wangu na mwinua kichwa changu.
4 Kwa sauti yangu namwita Bwana Naye aniitikia toka mlima wake mtakatifu.
5 Nalijilaza nikalala usingizi, nikaamka, Kwa kuwa Bwana ananitegemeza.
6 Sitayaogopa makumi elfu ya watu, Waliojipanga juu yangu pande zote.
7 Bwana, uinuke, Mungu wangu, uniokoe, Maana umewapiga taya adui zangu wote; Umewavunja meno wasio haki.
8 Wokovu una Bwana; Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
← Rudi kwenye faharasa