Zaburi - Sura 82

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150
← Iliyotangulia Inayofuata →
1 Mungu asimama katika kusanyiko la Mungu; Katikati ya miungu anahukumu.
2 Hata lini mtahukumu kwa dhuluma, Na kuzikubali nyuso za wabaya?
3 Mfanyieni hukumu maskini na yatima; Mtendeeni haki aliyeonewa na fukara;
4 Mwokoeni maskini na mhitaji; Mwopoeni mikononi mwa wadhalimu.
5 Hawajui wala hawafahamu, hutembea gizani; Misingi yote ya nchi imetikisika.
6 Mimi nimesema, Ndinyi miungu, Na wana wa Aliye juu, nyote pia.
7 Lakini mtakufa kama wanadamu, Mtaanguka kama mmoja wa wakuu.
8 Ee Mungu, usimame, uihukumu nchi, Maana Wewe utawarithi mataifa yote.
← Rudi kwenye faharasa