Zaburi - Sura 120

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150
← Iliyotangulia Inayofuata →
1 Katika shida yangu nalimlilia Bwana Naye akaniitikia.
2 Ee Bwana, uiponye nafsi yangu Na midomo ya uongo na ulimi wa hila.
3 Akupe nini, akuzidishie nini, Ewe ulimi wenye hila?
4 Mishale ya mtu hodari iliyochongoka, Pamoja na makaa ya mretemu.
5 Ole wangu mimi! Kwa kuwa nimekaa katika Mesheki; Na kufanya maskani yangu Katikati ya hema za Kedari.
6 Nafsi yangu imekaa siku nyingi, Pamoja naye aichukiaye amani.
7 Mimi ni wa amani; Bali ninenapo, wao huelekea vita.
← Rudi kwenye faharasa