Zaburi - Sura 128

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150
← Iliyotangulia Inayofuata →
1 Heri kila mtu amchaye Bwana, Aendaye katika njia yake.
2 Taabu ya mikono yako hakika utaila; Utakuwa heri, na kwako kwema.
3 Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao, Vyumbani mwa nyumba yako. Wanao kama miche ya mizeituni Wakiizunguka meza yako.
4 Tazama, atabarikiwa hivyo, yule amchaye Bwana.
5 Bwana akubariki toka Sayuni; Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako;
6 Naam, ukawaone wana wa wanao. Amani ikae na Israeli.
← Rudi kwenye faharasa