Zaburi - Sura 61

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150
← Iliyotangulia Inayofuata →
1 Ee Mungu, ukisikie kilio changu, Uyasikilize maombi yangu.
2 Toka mwisho wa nchi nitakulilia nikizimia moyo, Uniongoze juu ya mwamba nisioweza kuupanda.
3 Kwa maana ulikuwa kimbilio langu, Ngome yenye nguvu adui asinipate.
4 Nitakaa katika hema yako milele, Nitaikimbilia sitara ya mbawa zako
5 Maana Wewe, Mungu, umezisikia nadhiri zangu. Umewapa urithi wao waliogopao jina lako.
6 Utaziongeza siku za mfalme, Miaka yake itakuwa kama vizazi vingi.
7 Atakaa mbele za Mungu milele, Ziagize fadhili na kweli zimhifadhi.
8 Ndivyo nitakavyoliimbia jina lako daima, Ili niondoe nadhiri zangu kila siku.
← Rudi kwenye faharasa