Zaburi - Sura 67

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150
← Iliyotangulia Inayofuata →
1 Mungu na atufadhili na kutubariki, Na kutuangazia uso wake.
2 Njia yake ijulike duniani, Wokovu wake katikati ya mataifa yote.
3 Watu na wakushukuru, Ee Mungu, Watu wote na wakushukuru.
4 Mataifa na washangilie, Naam, waimbe kwa furaha, Maana kwa haki utawahukumu watu, Na kuwaongoza mataifa walioko duniani.
5 Watu na wakushukuru, Ee Mungu, Watu wote na wakushukuru.
6 Nchi imetoa mazao yake MUNGU, Mungu wetu, ametubariki.
7 Mungu atatubariki sisi; Miisho yote ya dunia itamcha Yeye.
← Rudi kwenye faharasa