Zaburi - Sura 149

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150
← Iliyotangulia Inayofuata →
1 Haleluya. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Sifa zake katika kusanyiko la watauwa.
2 Israeli na amfurahie Yeye aliyemfanya, Wana wa Sayuni na wamshangilie mfalme wao.
3 Na walisifu jina lake kwa kucheza, Kwa matari na kinubi wamwimbie.
4 Kwa kuwa Bwana awaridhia watu wake, Huwapamba wenye upole kwa wokovu.
5 Watauwa na waushangilie utukufu, Waimbe kwa sauti kuu vitandani mwao.
6 Sifa kuu za Mungu na ziwe vinywani mwao, Na upanga mkali kuwili mikononi mwao.
7 Ili kufanya kisasi juu ya mataifa, Na adhabu juu ya kabila za watu.
8 Wawafunge wafalme wao kwa minyororo, Na wakuu wao kwa pingu za chuma.
9 Kuwafanyia hukumu iliyoandikwa; Hiyo ndiyo heshima ya watauwa wake wote. Haleluya.
← Rudi kwenye faharasa